DAR ES SALAAM COLLEGE OF HOTEL AND BUSINESS STUDIES

DAR ES SALAAM COLLEGE OF HOTEL AND BUSINESS STUDIES
P.O BOX 40015, TANZANIA EAST AFRICA NAFASI ZA MASOMO YA HOTEL, TOURISM& BUSINESS CERTIFICATE AND DIPLOMA COURSE IN 1. Hotel Reception and front office 2. Food science and Beverage services 3. Tourism and Travel studies 4. Hotel House keeping 5. Food Production Cooking and Bakery 6. Clearing and forwarding 7. Computer studies and Maintenance 8. Accounting 9. Business Administration 10. Procurement & Supply 11. Human Resource Chuo kimesajiliwa NACTE Reg No (BMG/054P) KwaMawasilianozaidi: 0713-601763, 0755-823449, 0789-0447442, 0767-929110

HATIMAYE ROSE MUHANDO APATA MPINZANI WAKE


ROSE Muhando amekuwa akitamba katika ulimwengu wa nyimbo za injili kwa miaka kadhaa sasa bila kujitokeza kwa mpinzani wake wa kweli, lakini ujio wa mwimbaji mwingine wa injili Sarah Bagumhe (Pichani) kunaweza kuleta ushindani wa kweli.

Sarah ameanza kutamba katika muziki wa Injili jijini Mwanza na sasa anakaribia kuiteka Tanzania kwa ujumla, amepiga hodi visiwani Zanzibar na anatarajia kufanya tamasha kubwa huko Zenji.

Mratibu wa maonyesho yake Paskal Linda amesema ujio wa mwanadada huyo katika injili na dhahili Rose Muhando amepata mpinzani wake, 'Kusema kweli Sarah Bagumhe anajua kutunga na kuimba hivyo ushindani wa kweli unaweza kuwepo', alisema Linda.


Msanii huyo tayari amerekodi album yake ya audio na video inayokwenda kwa jina 'Ni vizuri kumshukuru Mungu', albam hiyo inajumuhisha nyimbo nane, nyimbo zilizomo ni pamoja na Ni vizuri kumshukuru Mungu ambayo inabeba jina la albamu hiyo, ufanane na nani ?, Mwoyo gwange, nena rohoni, nipe maji, tulina omukwano, nipe nguvu na tupapoomba.

Nyimbo zote zimefanywa na kampuni ya GTC Media ya Kisumu nchini Kenya, akizungumza zaidi Sarah amesema 'kwanza namshukuru Mungu kwa kumaliza mwanzo wa kazi hii pia na wote walio nisaidia kufika mpaka hapa, pia naomba sana wapenzi wa injili wasubirie kwa hamu video ya 'Ni vizuri kumshukuru Mungu', ambayo itakuwa ni nzuri kuliko na inatarajia kuwa hewani mwezi ujao` alisema. www.palimude.blogspot.com