DAR ES SALAAM COLLEGE OF HOTEL AND BUSINESS STUDIES

DAR ES SALAAM COLLEGE OF HOTEL AND BUSINESS STUDIES
P.O BOX 40015, TANZANIA EAST AFRICA NAFASI ZA MASOMO YA HOTEL, TOURISM& BUSINESS CERTIFICATE AND DIPLOMA COURSE IN 1. Hotel Reception and front office 2. Food science and Beverage services 3. Tourism and Travel studies 4. Hotel House keeping 5. Food Production Cooking and Bakery 6. Clearing and forwarding 7. Computer studies and Maintenance 8. Accounting 9. Business Administration 10. Procurement & Supply 11. Human Resource Chuo kimesajiliwa NACTE Reg No (BMG/054P) KwaMawasilianozaidi: 0713-601763, 0755-823449, 0789-0447442, 0767-929110

Alikiba: Diamond hawezi kuziba nafasi yangu

MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba, amesema msanii mwenzake wa muziki huo, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ hawezi kuziba nafasi yake. Kauli hiyo ya Alikiba imekuja baada ya kutakiwa kuelezea alivyojipanga katika ujio wake mpya katika muziki huo kutokana na kuonekana kwamba nafasi
ambayo alikuwa nayo kwa miaka ya nyuma sasa inashikiliwa na Diamond.
“Hakuna aliyechukua nafasi yangu katika tasnia ya muziki, yani kama ni kiti basi kina vumbi, ninachokifanya ni kukipangusa na kukikalia tena, kila mmoja ana nafasi yake, hivyo sijaona bado aliyechukua nafasi yangu,” alisema Alikiba.
Alisema kuwa alikuwa ameamua kupumzika tu sio kwamba anaogopa ushindani, na kuongeza kuwa sasa yupo katika hatua za mwisho za maandalizi ya ngoma yake mpya inayojulikana kwa jina la ‘Dar es Salaam’ ambayo ndani yake ameelezea jinsi vijana wanavyojiingiza katika janga la dawa za kulevya.
Alikiba alisema ameamua kutoa wimbo wa kuwahamasisha vijana wenzie waachane na utumiaji wa dawa za kulevya kwani zinapoteza wengi na hazina faida yoyote. Anaamini kwa kufanya hivyo kuna ambao wataepuka.