DAR ES SALAAM COLLEGE OF HOTEL AND BUSINESS STUDIES

DAR ES SALAAM COLLEGE OF HOTEL AND BUSINESS STUDIES
P.O BOX 40015, TANZANIA EAST AFRICA NAFASI ZA MASOMO YA HOTEL, TOURISM& BUSINESS CERTIFICATE AND DIPLOMA COURSE IN 1. Hotel Reception and front office 2. Food science and Beverage services 3. Tourism and Travel studies 4. Hotel House keeping 5. Food Production Cooking and Bakery 6. Clearing and forwarding 7. Computer studies and Maintenance 8. Accounting 9. Business Administration 10. Procurement & Supply 11. Human Resource Chuo kimesajiliwa NACTE Reg No (BMG/054P) KwaMawasilianozaidi: 0713-601763, 0755-823449, 0789-0447442, 0767-929110

Darasa awapa tano mashabiki


 Sharifu Thabit ‘Darasa’MSANII wa muziki wa Hip Hop nchini, Sharifu Thabit ‘Darasa’, amewashukuru mashabiki wa muziki huo, kwa kumpa sapoti katika muziki wake tangu alipoingia katika tasnia hiyo.
Akizungumza Tanzania Daima jijini Dar es salaam jana, Darasa alisema, tangu anaanza muziki amekuwa akipata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki na wadau wake ndani na nje ya nchi, hivyo ni kitu cha kujivunia kwake.
Darasa ambaye yuko katika kundi la Classic Music Group (CMG), ambalo lipo chini ya studio ya AM Records, kwa sasa anatamba na kibao chake cha
‘Sio Mbaya’, licha ya kupaya umaarufu kupitia vibao vingine kama, Sikati Tamaa, Nishike Mkono, Ukipenda Hauoni na nyinginezo.
Alisema, pia anashukuru kupata sapoti kutoka kwa mkongwe wa muziki huo nchini, Joseph Haule ‘Proffesor Jay’, kitu ambacho anajivunia.
“Nashukuru kupewa sapoti kutoka kwa nguli huyu, aliposikia wimbo wangu wa ‘Sikati Tamaa’ alinitafuta na kuzungumzia uwezo wangu katika vyombo mbalimbali vya habari, kiukweli ni kitu ambacho najivunia sana,” alisema